Jukwaa la Kiswahili
Karibu kwenye jukwaa la jamii ya wapenzi wa Kiswahili kama wewe. Uliza maswali, jibu maswali ya wanajamii wenzako. Toa maoni au mapendekezo.
FASIHI SIMULIZI KATIKA ENZI ZA UTANDAWAZI
MATAPO YA FASIHI
NADHARIA YA FASIHI NA MAENDELEO YA FASIHI YA KISWAHILI
Nadharia ya U - Marx ni nadharia inayochambua mifumo ya kijamii huku ikiegemea zaidi katika chanzo cha tofauti zilizopo kati ya wenye nafasi na wanyonge kiuchumi katika jamii zetu. Marx anaamini kuwa tofauti hizi husababishwa na mabwanyenye kuwanyanyasa wachochole na hivyo kutumia nguvu za wachochole kujinufaisha wenyewe. Kazi za fasihi zinazoweza kuakisi nadharia hii ni pamoja na Kilio Cha Haki ya Al Amin Mazrui
-Mwita Jacob -5 days ago
MAANA YA USHAIRI
“ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa sanaa ya sanaa ya vina ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari.
Na Mathias Mnyampala anaeleza kuwa
“ ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale. Ndicho kitu kilicho bora sana katika maongezi ya dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa vina maalumu kwa shairi.
Katika maana hizi za ushairi kuna mambo kadhaa yanayoibuka. Kwanza kabisa, kipengele cha lugha kinatiliwa mkazo na washairi wote hao waliojaribu kueleza maana ya ushairi japo kwa mitazamo tofauti wakieleza kuwa shairi zuri halina budi kuwa na ufasaha wa lugha, maneno ya mkatomaalumu yenye lugha nyofu, tamu na laini, nzito yenye kunata.
Kwa ujumla,basi wanamapokeo hawana ugomvi wowote na washairi wakisasa kuhusu kipengele cha lugha. Wote wanakubaliana kuwa lugha ya ushairi haina budi iwe ya mkato na ya ufasaha.
Wanamabadiliko wanatoa maana ya ushairi hivi:-
Kezilahabi, anasema “ushairi ni tukio,hali au wazo ambalo limeonyeshwa kwetu kutokana na upangaji wa fasihi yenye mizani kwa kifupi ili kuonyesha ukweli fulani wa maisha”, naye M.M. Mlokozi anasema:-
“ ushairi ni mpangilio maalumu wa maneno fasaha yenye muwala, kwa lugha ya mkato, katika usemi, maandishi au mahadhi ya nyimbo ili kueleza wazo au mawazo kutunza au mahadhi ya nyimbo ili kueleza wazo au mawazo kutunza au kueleza jambo au hisi fulani kuhusu maisha ya binadamu kwa njia inayoburudisha na kugusa moyo. (Senkoro F. 1988)
Baada ya kuchunguza kwa kifupi kuhusu maana ya ushairi kufuatana na mawazo ya wataalamu wa fasihi ya kiswahili, maana inayoweza ikasadifu kueleza ushairi ni:-
“ ushairi ni utanzu wa fasihi utumiayo mpangilio wa lugha ya mkato ya kipicha na iliyopangwa kwa njia iletayo mapigo mahususi kufuatana na maudhui yahusikayo”