Nyimbo Katika Fasihi Simulizi


NYIMBO
Utanzu wa Fasihi Simulizi
KiingerezaSongs
PrevNext
Hadithi/NganoMaigizo


Nyimbo ni aina ya sanaa katika fasihi ambayo hutumia lugha teule, sauti na kiimbo maalum. Aghalabu nyimbo hutumia ala za mziki kama vile ngoma. Nyimbo zinaweza kuimbwa na mtu mmoja au zaidi. Wimbo hugawanywa katika beti na mishororo. Nyimbo nyingi huwa na kiitikio au mstari ambao hurudiwa rudiwa.

Sifa za Nyimbo


  1. Hutumia kiimbo au sauti maalum
  2. Huweza kuendamana na ala za muziki
  3. Huimbwa na mtu mmoja au watu wengi; wakati mwingine nyimbo huimbwa kwa kupokezanwa.
  4. Hutumia lugha ya mkato
  5. Hurudiarudia (kukariri) maneno ili kusisitiza ujumbe katika wimbo



Umuhimu wa Nyimbo katika Fasihi Simulizi


  1. Kuburudisha
  2. Kuelimisha, kufunza, kuonya, kuelekeza
  3. Kuliwaza
  4. Kusifia kitu au mtu katika jamii
  5. Kuunganisha jamii
  6. Kudumisha/kuhifadhi tamaduni za jamii
  7. Kukuza talanta na sanaa katika jamii
  8. Hutumika katika mbinu nyingine za fasihi kama vile hadithi



Vipera/Aina za Nyimbo

Kulingana na Muundo:


  1. Mashairi
  2. Maghani

Kulingana na Ujumbe/Maudhui:


  1. Nyimbo za Ndoa


    Nyimbo za harusi huimbiwa bwana na bibi harusi kuwapongeza na kuwapa heko kwa kufunga ndoa yao. Aidha nyimbo hizi huwapa wawili hao mawaidha ya kutunza familia na watoto wao ili waishi pamoja.
  2. Nyimbo za Jandoni/Tohara


    huimbwa na vijana wanapopashwa tohara. Nyimbo hizi huonyesha ushujaa, na kuashiria kutoka kwamba anayetahiriwa amekuwa mtu mzima sasa.
  3. Hodiya/Wawe


    Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa na watu wanapofanya kazi ili kuwatia bidii wafanye kazi bila kuhisi machofu.
  4. Kimai


    Nyimbo za Mabaharia - Hizi ni nyimbo za wanabahari wanaposafiri baharini.
  5. Nyimbo za Mazishi/Huzuni/Simanzi


    Hizi ni nyimbo za kuliwaza na kuwapa pole walioachwa na marehemu. Nyimbo hizi huwapa matumaini waombolezaji.
  6. Nyimbo za Kidini


    Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa kumsifia Mungu, kuomba au kutoa mafunzo ya kidini.
  7. Nyimbo za Kisiasa


    Hizi ni nyimbo za kuwasifia viongozi wa kisiasa
  8. Nyimbo za Kizalendo


    Nyimbo za huonyesha uzalendo kwa kusifia taifa/nchi
  9. Nyimbo za Mapenzi


    Katika nyimbo za mapenzi, mwimbaji huimba kwa kumsifia mpenzi wake hasa kwa urembo na tabia zake.



ushairi ni tanzu ya fasihi andishi ama fasihi simulizi
- baby young - 3 weeks ago

Ushairi ni utanzu wa fasihi simulizi(nyimbo) na pia utanzu wa fasihi andishi kwa sababu huandikwa na kuhifadhiwa vitabuni.
- Silah Rokito Chelimo - 2 weeks ago

Login to Comment